ENTERTAINMENT

Mpiga Picha wa Millard Ayo, Zuchy Afariki Katika Ajali

Mpiga Picha wa Millard Ayo, Zuchy Afariki Katika Ajali

Habari ya kusikitisha imetufikia kuhusu kifo cha Noel Mwingila, maarufu kama Zuchy, ambaye alikuwa mpiga picha na mwandishi wa habari wa @millardayo na @ayotv_. Zuchy alifariki dunia mapema Alfajiri ya leo baada ya kupata ajali ya pikipiki eneo la Makonde – Mbezi, jijini Dar es Salaam. Chanzo cha karibu kimeithibitisha habari hii.

RELATED; Amos & Josh Ft King Kaka – Baadaye

Zuchy anatambulika kama mmoja wa wapiga picha mahiri katika tasnia ya habari na matukio. Wasafi Media tunatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, na timu nzima ya Millard Ayo & Ayo TV kwa msiba huu mzito. Tunamuombea Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Leave a Comment