Uncategorized

Vitu 4 ambavyo vitakufanya upewe mapenzi zaidi na mpenzi wako

Vitu 4 ambavyo vitakufanya upewe mapenzi zaidi na mpenzi wako

Watu wengi siku hizi huwa wanaanza kuiwaza wikiendi pale tu jua la jumatano linapokuwa linaanza kuzama. Usije kuwalaunu watu hawa maana huwa ni kawaida.

Ni kawaida maana wikiendi ni siku ambazo watu wengi huweza kukutana na wawapendao bila kuwa na mashaka au mawazo mengine ya kiofisi au shughuli yoyote nyingine.

Mihangaiko na jinsi mambo yanavyokuwa bize kipindi hiki cha kiutandawazi na maendeleo ni vigumu mtu kuwaza mapenzi hasa katikati ya wiki.

Na huwa inatokea na ni mara nyingi wikiendi inafika ila unajikuta haupati mapenzi ya kutosha kama vile moyo wako unavyokuwa unatamani itokee, kwa wale ambao wangependa mambo mazuri ya kubomoa chaga za vitanda yatokee wikiendi hi, hizi hapa ni njia za kufata ili ufanikishe unayoyawaza.

1. Mnunulie mpenzi wako zawadi. 
Zawadi ni njia moja nzuri na inayoweza kukufanikishia mambo yako yakaenda utakavyo na kuvunja buyu la asali, tafuta zawadi nzuri ambayo unajua atapendezwa nayo, iwe gauni zuri au mkoba mzuri na mapenzi yaliyozidi kipimo yatakuwa yako mwisho wa wiki hii.

2. Mtoe mtoko sehemu nzuri. 
Wikiendi hii inaweza kuwa wakati mzuri wa kumtoa kwenye mtoko msichana wako, jaribu kutafuta sehemu nyingine tofauti na chumbani kwako na utaona mafanikio ambayo yatajitokeza, mkitumia siku mbili kwenye hoteli flani, mapenzi yatakuwa mengi kama vile mpo kwenye hanimuni, maana itakuwa kula, kunywa na mambo yetu yakifuata katika kipimo ukipendacho wewe kwa wikiendi nzima.

3. Umtaarishavyo vizuri kimahaba ndivyo utakavyo pewa mapenzi mengi na mazito zaidi. 
Je wewe ni kati ya wale wanaohisi mapenzi ni kitendo cha uume kuingia sehemu ya kike tu? Hapana, kitu cha kwanza unatakiwa umtengenezee hakshi ya mahaba, mpeti peti umfanye apate hamu kwa kumtaarisha kwa hali nzuri na kwa mitekenyo inayohitajika, mtayarishe bila haraka, mbusu mabusu ya hisia, mashavuni, kwenye midomo yake telemka taratibu mpaka apate raha duniani na mpe maneno matamu ya kumchanganya zaidi. Mambo yote haya ukiyafanya vizuri na ukamfanya apagawe hakika lazima na yeye atataka zaidi na wewe utapata yakutosha pia.

4. Mwachie Aongoze Mambo. 
Ukweli ni kwamba wanaume wengi huwa hujiangalia wao tu, hawataki kusikiliza japo hata kumuuliza mwenza wao naye angependelea nini, wanawake wanapenda sana akipewa nafasi ya kuamua ni spidi gani itumike mkiwa kitandani, kwa hio badala ya wewe kufanya bila kumuuliza mwenzio anataka nini na mfanye mapenzi kwa staili gani, mwachie nae aamue, mwambie hii siku ni ya kwake yeye, wewe kwake ni mtumwa tu, atatakacho upo kwa ajili ya kumtimizi, muulize umshike wapi na umfanye nini maruhani yake yapande, muulize angependelea kasi gani ya ufanyaji wa mapenzi, mnongoneze maneno matamu ya kumpagawisha.

Kama akitaka yeye ndo awe juu, na wewe uwe chini mwache dada wa watu afanye yake, ajifikishe mwenyewe apendako na kama ni kileleni, haya! jinsi atapokuwa anasikia raha na kufurahi ndipo atakapo hitaji zaidi na wewe mwisho wa siku kupewa zaidi.

Na hapo mpaka wikiendi iishe lazima uwe mwepesi kama bendera.

Leave a Comment