LYRICS

Lava Lava – Basi Tu LYRICS Ft Mbosso

Lava Lava – Basi Tu LYRICS Ft Mbosso

GET AUDIO HERE

GET VIDEO HERE

Lava Lava – Basi Tu LYRICS Ft Mbosso

Siku hizi hanipigii
Hata akikuta missed call zangu
Simu hashiki na akishika
Anauliza nani mwezangu

Mara anakata
Mara simu hewani haongei
Namaliza vocha
Anajizima data eti amepanda bei
Kunifanya ndodocha

Najitumisha message
Mara mbili mbili
Anafungua anasoma
Majibu hayarudi eh eh eh

Ila kwa Whatsapp page
Zaonyesha tiki mbili
Kujifanya hajaona
Ili mradi kusudi na kunidharau

Ananiringia ringia
Ananiringia ringia
Siku hizi ananiringia ringia
Ananiringia ringia

Anajua nampenda (Basi tu)
Anafanya kusudi kuniumiza (Basi tu)
Ili mradi kuniliza (Basi tu)
Anafanya kusudi kuniumiza (Basi tu)
Ili mradi kuniliza

Aah…aah…aah

[Mbosso]
Na dhalia hainaga suu
Yaliyosemwaga ya kale
Kufurahia kunguru nafuu
Wakigombana mbalale

Moyo unawaka moto kifuu
Yanichoma maumivu mshale
Enyi malaika mlio juu
Shusheni amani itawale

Nayamaliza madhehebu
Kusomewa madua
Mbolea imekausha mbegu
Imeshindwa chipua

Mtazame nampenda kwa sana
Leo unanifanya mi nalia
Ina maana ndo nimechokwama
Au jamaa sina fungu kwenye dunia

Najitumisha message
Mara mbili mbili
Anafungua anasoma
Majibu hayarudi

Ila kwa Whatsapp page
Zaonyesha tiki mbili
Kujifanya hajaona
Ili mradi kusudi na kunidharau

Ananiringia ringia (Ananiringia)
Ananiringia ringia (Ananidengulia)
Siku hizi ananiringia ringia
Anairusha rusha roho yangu
Ananiringia ringia

Anajua nampenda (Basi tu)
Anafanya kusudi kuniumiza (Basi tu)
Ili mradi kuniliza (Ila basi tu)
Anafanya kusudi kuniumiza (Basi tu)
Ili mradi, ila nenda

Nenda mwambie asante
Mwambie asante
Nenda mwambie asante
Mwambie asante

Nenda mwambie asante
Mwambie asante
(Kanifunza maumivu nilikuwa siyajui)
Nenda mwambie asante
Mwambie asante
(Ustahimilivu nisilipize uadui)

(Kwa Mix Lizer)

Also check more tracks from Lava Lava;

Leave a Comment