LYRICS

Lyrics Rostam – Kaka Tuchati

Lyrics Rostam - Kaka Tuchati
Lyrics Rostam – Kaka Tuchati: It’s a brand new day and we are happy to bring you hizi Lyrics toka kwa Rostam Kaka Tuchati. Enjoy!

DOWNLOAD MP3

Oooii naona mtandao unakatika
Upo kimya sana mkato au kunde imevunjika
Na mtanyooka roundi hii 
Na hivi huwezi bila mimi?

Najikuta Jay Z oya unarudi lini?
Kaka huku wamefunga mipaka
Ila tiketi nilikata nirudi kabla ya pasaka
Rudi ugeuze kisu sio
Mwana wa kulitafuta mwana wa kulipata
Round hii sio nunio, daraja la mpasu

Kumekucha hivi saa ngapi huko nipe takwimu
Nimeamka nishaweka bundle namngoja Umi mwalimu
Anapambana yule dada
Tanga nimewavulia kofia wametoa sanitizer za iliki
Yaani ukipaka unanukia

Hehehe Corona nishai yaani Bongo kila mtu daktari
Masai kachemsha maji ya mpapai kanywa na sukari
Guza hadi maski wanafua sijui ni nani kawafundisha
Huku kuna dada kajifukiza mashetani kayapandisha

Tueke siasa kando unajua uchumi unashuka
Sio Bongo tu hadi ng’ambo watu wamefunga maduka
Hapa nawaza pesa ya bango benki walokopa wanajuta
Tukisema tukae ndani na hii njaa si tutakufa

Hali inatisha na umasikini, tunaoumia ni sisi
Yaani bora ufe kwa Ukimwi angalau utaandika urithi
Kwa iyo hamna bata, sio kidimbwi sio tipsi
Kaka madanga yamekata so hazitimbi hizo piece

Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
Alpha na Omega nani kama wewe
Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
Alpha na Omega nani kama wewe

Hivi unakaa jimbo gani au Marekani
Unajikinga vipi maana vifo vingi hadi siamini (Mmmh)
Au umesharudi ipo zako Horohoro nini
We bwana hebu niache mi nimeze chloroquine

Umenikumbusha kweli Chloroquine ni dawa?
Bado inafanyiwa uchunguzi ila haijadhibitishwa
Ingawa ukinywa haitohatarisha ndio maana bado wanaigawa
Mi ninakunywa maana nilishika uso kabla ya kunawa

Eti unaweza ukawa nayo na usionyeshe dalili?
Ewaah! Uko sahihi, na kingine kuhusu hili ni kwamba
Mgonjwa wa Corona unaweza usimtambue kwa macho
So mtu yeyote unayemuona mpe mita mbili toka kwako

Na hiko kiVansileka ndo kinini baba wawili?
Ni ventilator, ni mashine ka mapafu ya nje ya mwili
Mmmh sijaelewa hebu nieleweshe kuhusu hili
Naskia vinauzwa ghali basi viwe vingi Muhimbili 

Okay, kirusi cha Corona kinashambulia mapafu
Ndipo zinaanza homa, kifua alafu 
Unashindwa kupumua na mwili unahitaji tafu
Ventilator huingiza hewa na kuitoa iliyo chafu

Tuepuke mikusanyiko ikibidi tukae ndani
Tumeambiwa tujifukize hivi ni dawa unadhani?
Ngoja kwanza, hivi fumigation (Mmmmh mmh)
Baba ile inaua mende eti (Hahaha wacha utani)

Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
Alpha na Omega nani kama wewe
Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
Alpha na Omega nani kama wewe

Maisha ya upweke yanasumbua ila siku zinapita
Yule mkewe itunze pete 
Mtayamaliza na uhakika kaka 
Ila hatua dua haina haja ya kusikitika

Ila navyokujua hujazini miezi sita?
Kiukweli mi mwaminifu ingawa jogoo anawika
Mama Ivan mbabaifu haku-cheat una uhakika?
Kuna mchezaji wa Yanga namwona anapita pita

Nitamkata kata mapanga yaani namuua na namzika
Oyaah wape nyumbani basi pesa ya matumizi
Kaka nitoe wapi na show hakuna siku hizi?
Hali imekuwa ngumu hakuna pesa kila kona

Kila mtu unayemdai naye anasingizia Corona
Mbona sasa wanafunga shule na vyuo alafu bar hawafungi
Mzazi atamlindaja mtoto na akirudi yuko tungu?
Polisi India wanapiga watu wakisongamana

Wao barakoa hawana, jua defender wamebanana
Sasa wanatukusanya kutuambia tusikusanyike
Ila wauguzi wanajitoa sana, dah Mungu awalipe
Wapinzani mnatangaza vifo walopona hamwatangazi

Ah-ah wanasema wangeweka takwimu za wazi ingekuwa kizazi
Kwa hivyo lockdown hakuna alafu umeona text niliyotuma?
Ipi kwenye group mbona inbox hakuna?
Ah naskia (Nini?) koyuzeka mbochi
Maana uliko uliko usiongee sana inatosha
Hadi papai lina Corona dah (Kaka tuchati)
Mmmh ina mbuzi vipi? (Eeh eh kaka tuchati)
Mwili umekufa ngazi (Kaka tuchati)
Poa mwanangu tuendelee kujifukiza 

(Tongwe Records, Bin Laden)

DOWNLOAD MP4

Lyrics Rostam – Kaka Tuchati

Roma Instagram: https://www.instagram.com/roma_zimbabwe/

Leave a Comment