MAKALA

SMS 1000 za mapenzi kwa yule umpendaye

SMS 1000 za mapenzi kwa yule umpendaye
 

Mimi ni mkimbizi wa mapenzi na nimekimbilia kwako,

sikwenda mwingine wewe ndiye chaguo langu,
nipe hifadhi moyo mwako mwenzio sinayo hali.
nihifadhi peke yangu nami nitakuhifadhi moyoni mwangu.
 
**********
 
Nakutakia usiku mwema kwako wewe wangu kipenzi,
uote njozi njema, na uniote nami pia.,
usiku huu uwe wenye baraka kwako nami dua kukuombea,
malaika wa kheri wazunguke kitanda chako.usiku mwema.
 
**********
 
Mapenzi ni kama mti huchanua yanaponyeshewa,
hunawiri yanapolelewa, na hutoa matunda pindi yanapo thaminiwa,
gharama la tunda litokalo mtini hapo hutegemeana na ubora wake.
nasi tulifanye penzi letu liwe bora,na lenye kuthaminiwa.
 
*********
 
Pendo ni dawa ya kidonda cha moyo, huleta faraja ulipokata tamaa,
yaleta furaha ulipokwa unaraha, huleta thamani iliyopotea,
huleta amani pasipo na amani, nakupa langu pendo kwa sababu nakupenda sana,
usisahau kumeza kwani utaharibu dozi.
 
*************
 
Maneno huanza na ABC. Namba 123. Muziki na do re mi… na
mapenzi huanza na mimi na wewe.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Mvua na jua haviwezi kuwa pamoja, usiku na mchana
hazigongani, lakini mimi na wewe, hata wasemaje,
‘tunafiti’ kuwa pamoja.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Kuna bahari kati yetu. Misitu na milima inatutenganisha,
mimi si ‘Supamani’ lakini nipe sekunde moja nitavuka nchi
nyingi kukutumia mapenzi yangu. Umeipata hiyo?
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Natamani ningekuwa chozi jichoni mwako ambapo ningetelemka
na kuishia midomoni mwako, lakini kamwe sitamani uwe chozi
jichoni mwangu nitakupoteza kila muda niliapo.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Naweza kuishiwa ujumbe wa kukutumia. Naweza kuishiwa utani
pia. Naweza kuishiwa chaji lakini moyo wangu hauwezi
kukosa nafasi ya kukuweka.
 
     *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Penzi, maisha yangu yote nimesoma juu ya neno hili,
nimeota juu yake, nimelilia, nimelihitaji. Sasa pamoja
nawe nimelipata.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Kila mtu anataka kuwa jua linalong’arisha maisha yako,
lakini ni afadhali niwe mwezi, ili nikuangazie wakati wa
giza ambapo jua limechwea na haliangazi tena.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Unaweza usione kamwe ni kwa kiasi gani ninavyokujali.
Unaweza usisikie ni kwa kiasi gani nilivyokushiba, unaweza
usihisi namna gani ninavyokukumbuka. Sababu ni moyo wangu
tu uliyoyaficha hayo.
 
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Kama busu ni maji ningekupatia bahari, kukumbatia ni
majani, ningekupa msitu. Mapenzi ni maisha ningekupa yangu
bure.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Ni ngumu kwa watu wawili kupendana wanapoishi Dunia
tofauti, lakini Dunia hizo zikutanapo na kuwa kitu kimoja,
hiyo ndiyo maana ya kuitwa wewe na mimi.
 
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Watu husema kwamba, awapo mtu mmoja tu akupendaye, maisha
hayajapoteza maana, kwa hiyo, ukijihisi mpweke hauhitaji
kuishi nikumbuke mimi.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Watu waliniambia ninaweza kufanya chochote kama tu
nitaweka mawazo yangu juu ya hicho kitu. Lakini kila
nikijitahidi unaipoteza akili yangu
 
*°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Furaha yangu kubwa ni kuliona tabasamu lako, kujua uko na
furaha, na kuhisi upendo wako. Najua kuwa maisha mara
nyingine huwa ni makatili, na hiyo ni sababu niko hapa
kukuonyesha kuwa maisha yanaweza kuwa mazuri kama kuna mtu anayekujali.
 
        *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Chuki huharibu akili; mapenzi huitibu. Umeitibu akili yangu.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Kumjali mtu ni rahisi, lakini kumfanya mtu akujali ni
vigumu, nashangaa umewezaje kunifanya nikujali?
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Nitafute wakati una huzuni, nitafute wakati hamna wa
kukusikiliza. Sijali kama mimi ni kimbilio lako la mwisho,
bali sipendi ulie peke yako.
 
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Ningependa siku moja utamani sana kuwa na mimi, na
uhangaike sana kunitafuta, ili ujue ni kwa kiasi
ninavyotamani kuwa nawe sasa.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Kila unachokifanya natamani niwepo, nikitumainia kila
ndoto yako itimie kila muda na sehemu, niwepo nikikutakia
mafanikio mema kwasababu nakujali.
 
*°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
 
Kama ungekuwa kidonda kwenye moyo wangu, ningekiacha na
maumivu yake ndani yangu.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Kusumbuliwa na mlio wa simu yako, humaanisha kuwa muda
fulani, mahali fulani, kuna mtu anakufikiria muda huu, na
huyo ni mimi mara zote nakujali.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Nimekuapata! Kama unanichukia, nipige mshale, lakini
tafadhali si moyoni sababu hapo ndipo wewe ulipo.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Naweza kukuazima mabega yangu upande, masikio yangu
usikilizie mikono yangu ushikie, miguu yangu, utembelee,
lakini si moyo wangu kwani tayari unao wewe.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Lazima utakuwa mwizi sababu umeiba moyo wangu, umechoka
sababu unakimbia mara zote akilini mwangu, na labda mimi
sina shabaha sababu mara zote nikikulenga nakukosa.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Mpenzi kwa mara ya kwanza nilipokuana niliogopa kukuambia,
hata nilipokuambia niliogopa kukupenda, nilipokupenda sasa
naogopa mno kukupoteza. Kusema kweli siko tayari kukukosa
katika maisha yangu.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Wanasema mtu huanguka katika mapenzi mara moja, jambo
ambalo mimi naliona si la kweli kwa maana kila
ninapokutazama najikuta nakupenda tena na tena.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Mpenzi wangu kukutana nawe ilikuwa ni bahati, kukuchagua
kuwa rafiki yangu ilikuwa ni maamuzi yangu, lakini
kuanguka kwenye penzi lako haikuwa hiyari yangu. Umeniteka
moyo na akili yangu pia.
 
     *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Imani hufanya mambo yote yawezekane, Matumaini hufufua
yaliyopoteza uhai, lakini mapenzi hufanya mambo yote
yaonekane mazuri. Sina linalonihuzunisha maishani mwangu
kwa kuwa tunapendana!
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Mpenzi wangu T tambua kuwa ulimwengu tunaoishi una mambo
muhimu matatu. Jambo la kwanza ni kumpata umpendaye, la
pili ni kupata atakayekupenda la tatu ambalo ni kubwa
kuliko yote ni kwa jambo la kwanza na la pili kuungana pamoja.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Ni vigumu kumpata mwenye mapenzi ya kweli na zaidi yule
atakayekuwa tayari kukupenda zaidi, hivyo nafasi
inapopatika si busara kuichezea tudumishe penzi letu
laazizi wangu.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Nakupenda mpenzi W nafasi uliyotawala moyoni mwangu ni
kubwa, hakuna ambaye anaweza kufikia uhodari wako, wewe ni
mtu muhimu sana maishani mwangu.
 
     *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Nakupenda sana mwandani wangu ndiyo maana moyo wangu
hupatwa kidonda ninaokuona na mwingine hasa anapokuwa hana
sifa, nahisi kama anakutumia wewe kama mdori wake wa
kumfurahisha. Uwe makini ua la moyo wangu.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Nakupenda mpenzi wangu, sifikirii kitu chochote zaidi yako
na kwa kuwa nakupenda sipendi kuwa na urafiki hata na
msichana kwani atakuwa anabana nafasi niliyokuwekea wewe.
Noamba unipende nami nakupenda kila sikunde inayopita
maishani mwangu. Mwaaaaaaaaa
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Penzi lako ndiyo pumzi yangu nawezaje kukuacha laazizi,
ina maana nife??? Siwezi kukuacha nakupenda. Nitakupenda
mpaka mwisho wa uhai wangu.
 
*°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Asali wa moyo wangu, fahamu kuwa unaweza kuamini kwamba
mwanga wa nyota unaweza kuunguza nyumba, jua linaweza
kusimama, lakini usiwaze hata siku moja kuwa naweza
kukuacha.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Nakupenda sana P tafadhari usinikasirikie, nimekukumbuka
nahitaji kukuona unipoze moyo wangu, njooo mwandani wangu
nakusubiri daktari wangu.
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Mpenzi unawafahamu maadui wa mapenzi yetu ? Ni wale rafiki
zako wanaokuletea maneno ya uongo, ndugu zako
wanaotugombanisha na wachawi wanotuotea mabaya,
tujihadhari tusiwape ushindi. Mapenzi yetu yadumu daima.
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Uchungu wa kifo hauna tofauti na maumivu nitakayoyapata
ukiniachana, mpenzi usiniache nami siko tayari kukuacha
 
       *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
♥Watu wanao pendana daima hukumbukana!!! Na salamu
kusalimiana!!! Afya njema kutakiana!!! Huruma
huoneana!!! Kwenye shida husaidiana!!! Makosa
husameheana!!! Katika dhiki huvumiliana!!! Kila
jambo zur hupeana!!! Maneno mazur yaliyo jaa upendo
huambiana!!! Ushaur mwema hushauriana na njia
za mafanikio huonyeshana!!! Mbele ya madui hulindana!!!nai
ni mmoja katia ya wakupendao,hakika ni
mm wa kwanza kwanza wengine wanafata♥
 
      *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Yapitayo mdomoni yametokea moyoni ,uyaonayo hadharani
nimeagizwa na manani yakuridhishayo nafsini ni utamu wa
yakini.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Upendo wa moyoni ndiyo dhati niliyoamini amini kwa haya
nisemayo nakupenda wewe ndiyo kaburi nitakalozikwa nalo.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Nakupéndä mpènzi wèwè ùnåumuhimu mkubwa kwenye maisha
yangu kwani ukiniacha mpenzi utanisababishia kovu ambalo
halitapona .nakupenda sana
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mapigo yangu ya moyo huongezeka pindi nisipokuona japo kwa
dakika plz mpenzi kaa karibu yangu utulize mapigo
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Siku zote kwangu ni sherehe ni wewe unishereheshaye,ukweli
usio na kejeli mapenzi yako yanatii kiu yangu,moyoni
mwangu nimeridhia. . . .nakupenda daima mpenzi!
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mapenzi ni upepo,mimi sivumi na kupotea,mapenzi ni mahaba
sili nikamaliza,nikimaliza nitakula nini kesho?nakuahidi
kukupenda leo hata kesho ukiwepo na hata usipokuwepo.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
pongezi kwako mpenzi kuwa wangu mtetezi kwenye jahazi la
mapenzi,ufundi na ujuzi unao hasa tuwapo wawili
chumbani.penzi lako halichakai daima huzaliwa upya.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Nakupenda kwa kuwa umegundua thamani ya penzi langu
nakuahidi utafaidi utamu wa mapenzi yangu.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Wanafiki tusiwaombee kifo daima na milele washuhudie penzi
letu linavyozidi kukua,na tunavyopambana na mapito.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mpenzi usiende mbali nami,njoo ufaidi utamu usioisha
hamu,nitakupa mwili wangu ucheze nao hadi
asubuhi,nitakulisha unachokitaka,sitakubania kwani naogopa
wengine wanaweza kukupa. . . .njoo leo uniambie unataka
nini?
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mapenzi mazuri yanasifa zifuatazo,kuridhishana,kupeana
bila kubaniana,kubusiana,kuheshimiana,kujaliana,kusubiriana,kus
ikilizana.je utaweza kujifanyia yote hayo?nijibu mpenzi. .
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Ikiwa penzi langu kwako litakufa halitazikwa,ikiwa moyo
wangu ni mwandiko hautafutika na kama dhati yangu ni
machozi daima hayatokauka na wewe kwangu ni damu ngozini
haitochuruzika ila mishipani. . . .
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Anayekupenda ni mimi,watakaokutamani ni wengi,tafuta dunia
nzima penzi langu la kweli huwezi kulipata,penzi langu
kwako ni nuru daima halizimiki.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mpenzi usiende mbali nami,njoo ufaidi utamu usioisha
hamu,nitakupa mwili wangu ukeshe nao,nitakulisha
unachokitaka,sitakubania naogopa wengine wataniibia. .
.njo leo uniambie unataka nini?
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Nipe niridhike,nionjeshe usinilambishe,nikigonga
nikaribishe na penzi le2 2listawishe.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Utakuwa wangu wa maisha daima na penzi le2 litakuwa km
mfuko wa hazina,2talitunza km zaidi ya mboni la jicho.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Ni bora mnara ukitikisika kuliko kupata pengo lisilozibika
moyoni umeniachia jeraha lisilotibika na ufa
usiozibika.rudi mpenzi unautesa mtima wa moyo wangu.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Swt ulivyoumbika wengi wanateseka juu yako ,najua
wanakusumbua ni vema usiwakubalie, ukweli umebarikiwa
uzuri umeshushiwa na dhati ya penzi umetunukiwa nakupenda
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Wengi walisema penzi letu lisingedumu,lakini leo twawaacha
midomo wazi kwa misengenyo yao isiyo na maana ,tuendelee
kupendana,wanafiki roho ziwaume!
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Kama ni usafiri wewe ni gari salama,kama ni kiwanda wewe
ni namba moja ,kama ni maji kwako kuna chemchem,kama ni
mapenzi kwako nimefika,niahidi utakuwa nami siku zote
maishani mwangu.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Nilivyokutana nawe siku ya kwanza nilikupenda kwa
dhati,nikakueleza ukweli ukanikaribisha moyoni
mwako,siwezi kuchezea nafasi hiyo laaziz,nitakushika
daima.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Sura yako haifutiki usoni mwangu kirahic,ingawa upo mbali
nami lkn penzi lako bado nalikumbuka,hakuna anayeweza
kukata kiu yangu zaidi yako,nakupenda mpenzi.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Ucku ulalapo jua kuna m2 akupendaye,mchana uwajibikapo
tambua yupo anayekuwaza ,jioni uwapo mazoezini jua yupo
anayekuonea wivu,hata uwapo kwenye kumbi za burudani
tambua mwenzio nakulilia,usitoe penzi kangu akilini hata
km upo mbali nami!moyoni mwangu hutafutika milele!
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
 Hakika nimepata tabibu, maradhi yangu wajua kujyatibu,
napenda jinsi unavyonitibu, huna papara yaani ni taratibu,
mpenzi usijemuonyesha mwingine hizo zako zabibu, maswahibu
yakatayonisibu hakuna atakayeweza kuyatibu, nakupenda.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Joto ndio kitu nachotarajia kutoka kwao mke wangu
mtarajiwa, usisikilize maneno yakuambiwa, ni wewe tu
mwenye thamani kwangu katika hii dunia.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Kila niamkapo mawazo yangu huwa kwako na upepo uvumapo
huhitaji uwepo wako na hasa nikumbukapo kumbato lako,
nakupenda mpenzi.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Hakika wewe ndiye wangu mahabuba unayejua kunipa huba,
napenda unavyoniganda mithili ya ruba, nahahidi kukupa
mahaba yanayozidi shaba. Nakupenda.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Kila nikuonapo napata weweseko, yako miondoko si ya kitoto
na zaidi wajua kuweka mikogo, umeumbika si kitoto,
nahitaji uwe wangu mama watoto!
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Najua kuna vishawishi vingi sana uko ulipo, lakini nikiwa
moyoni mwako, siku hii itakuwa nzuri zaidi kwetu,
tupendane daima lahazizi…
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Wewe pekee upo moyoni mwangu, nitaendelea kukupenda siku
zote za maisha yangu! Katika siku hii ya wapendanao, wewe
ndiyo ua la moyo wangu!
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Weupe wa penzi lako ni kama mwezi angani.Ucheshi na mahaba
yako nifananishe na nini? Kupata mfano wako hatotokea
amini. Elewa mimiwako sikuachi asilani
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Penzi langu kwako ni la milele, nitakuhifadhi moyoni
mwangu siku zote za maisha yangu, uwe wangu nami niwe wako
daima, nakupenda dear…
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Hata kama nitajidanganya kwamba sikupendi, moyo wangu
umeganda kwako na hakuna dalili za kukuacha, wewe ni wangu
peke yako dear…
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Hata kama watasema mengi kiasi gani, kwako wewe
nitaendelea kuwa mpole, maana nakupenda sana…
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Niseme nini ujue nakupenda? Nifanye nini ujue nakupenda?
Nikuite jina gani ujue ni wewe peke yako upo moyoni
mwangu? Hakika hakuna ila moyo wangu ndio unaosema kuwa
nakupenda, niamini mpenzi
 
   *°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Upendo ni jibu kwamba kila mmoja anataka. . . .
upendo ni lugha ,kwamba kila mmoja anaongea,
upendo hauwez kununuliwa, na isiyo kadirika na ya bure,
upendo kama uchawi safi,ni siri ya maisha matamu nakupenda mpenzi
 
*°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
“Mimi sitaki kuwa kila kitu kwa kila mtu, lakini napenda
kuwa kitu kwa mtu.na mtu mwenyewe ni wewe”
nakupenda laazizi
“Kama mimi nilikuwa na maua  kila wakati
mawazo yangu
yangekuwa juu yako,nisingefikiri wa kumpa mwingine kabla
yako je wewe ungekuwepo nayo
 ungempa nani kwanza? “
 
*°·.¸¸.°  ♥  °·.¸¸.°*
 
Ningependa nikuambie neno ambalo halina gharama na
likutumiwa vibaya halina maana wala thamani. neno hilo
haliandikiki kwenye karatasi wala hata halitamkiki ila tu
Linatokea Bila kujua na halina sababu.neno hilo mi
mwenyewe silijui ila ndo linatufanya tuwe pamoja Japo tupo
Kasi Na Kusi. Nakupenda sana Dear
 
      •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Naukunjua moyo wangu huishi milele maishani ,nafungua
nafsi nikupende wewe pekee,nafunga milango ya moyo wangu
ili kutokupokea ugeni wowote wa moyo zaidi yako
mpenzi.nakupenda sana laazizi
 
      •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Sipo tayari kuukabidhi moyo wangu kwa mwingine zaidi
yako,wewe ni wa pekee maishani mwangu mwenye kujua hisia
moyoni mwangu mpenzi nipende daima pendo lako nitalienzi, nakupenda
 
     •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mapenzi si pombe  lkn yanalewesha, wala si kidonda  lakini
yanatonesha,wala si maradhi lakini yanaumiza, wala  si
njaa lakini yanakondesha ,mapenzi ni uvumilivu kwa
unaempenda
 
      •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mapenzi ni safari=unifanye nauli ya moyo, mapenzi ni
maradhi=unifanye daktari ni kutibu maradhi yako,mapenzi ni
kiu=niwe maji jangwani,mapenzi ni chakula=nikulishe
maishani mwako na uwe asali moyoni mwangu
 
       •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Wengi hupenda fanta kwa ladha yake,wengine hupenda
pilipili kwa muwasho wake,wengine hupenda asali kwa utamu
wake ila mimi nakupenda wewe kwa upendo wako.
 
      •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Nimetuma ndege wangu auzunguke ”moyo” wako kwa ” upendo
”  auguse ”uso” wako kwa ”faraja” na mwisho
akunong’oneze sikioni taratibu kuwa nakupenda.
 
        •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Mapenzi ni utoto,deka ulie nitakubembeleza,mapenzi ni
zawadi tabasamu nibusu niambie kiasi gani unanpenda,naweza
kusema asilimia kubwa jina lako limezunguka kuta wa moyo
wangu.kamwe jina lako haliwezi kufutika.nakupenda sana
 
      •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Teke la kuku halimuumzi mwanaye sawa na dhati ya mapenzi
haiumzi moyo wa ampendaye,tugombane sasa hivi tupatane
badaye,najua hakuna wasiogombana ,kama wapo siku
wakigombana wataachana.
 
     •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Yapitayo mdomon yametokea moyon,uyaonayo hadharani
nimeagizwa na manani yakuridhishayo nafsini ni utamu wa
yakini.
 
     •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Nakupenda sana mpenzi wangu ,we ndo wa pekee mwenye kujua
furaha ya moyo wangu nikiwa na majonzi huwa upo karibu
nami,nikiwa na furaha huja kushea nami,ahsante wangu
tabibu ,we ndo wangu wa manani.
 
     •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Kila niamkapo mawazo yangu huwa kwako na upepo uvumapo
huhitaji uwepo wako na hasa nikukumbukapo kumbato
lako,nakupenda mpenzi
 
     •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Furaha yangu ni kuwa nawe kwani u zaid ya mboni
yangu,najisifu kuwa nawe maishani mwangu naamini itatokea
kutokuwa mbali nawe mpz wangu,unisahaulishe machungu na
karaha za huu ulimwengu .nakupenda dia
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
>>———>>> Mshale huu unamtafuta mtu muhimu sana ktk
maisha yangu na kama umekutana nao
 usiukwepe uache
uchome Moyo wako gharama
 za matibabu juu yangu.
 
•·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Sioni zawadi ya kukupatia kwa mapenzi
unayonipatia, moyoni nimekuridhia wewe
pekee penzi langu daima kukupatia nakupenda
 
         •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Hakika kama ni mume MUNGU kanipatia,kuwa nawe najiona
kama malkia ,nakupenda mpz na daima nitaenzi penzi lako.
 
      •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•
 
Nina habari nzuri nataka kukuambia kuna mgeni leo kaja
kunitembelea,nguo nyekundu amevalia yaani!utamu wako kwa
sasa siwezi kukupatia kwa maana mgeni kashakuharibia nakupenda dear
 
        •·.·°¯`·.·•*•·.·°¯`·.·•

1 Comment

Leave a Comment